FEDHA NA UTAWALA

    Utangulizi

    Idara ya Utumishi na Utawala ni moja ya Idara za TUICO inayohusika na watumishi wa TUICO na Utawala. Idara hii inahudumia wafanyakazi wote wa Chama katika masuala ya Rasilimali watu na Utawala

    Kazi za Idara

    Kazi zinazosimamiwa na Idara hii ni kama ifuatavyo;

    1. Kubuni na kupanga mahitaji ya Rasilimali watu

    2. Kusimamia nidhamu za Watumishi wote

    3. Kutoa ushauri katika mashauri ya kinidhamu

    4. Kufanya tathmini ya ufanisi wa Watumishi

    5. Kushughulikia mambo ya kikazi ya Watumishi

    6. Kupandisha vyeo, mishahara, likizo na fidia kwa Watumishi

    7. Kuthibitisha kazini Watumishi

    8. Kutoa Elimu na mafunzo kwa Watumishi

    9. Kutoa huduma ya usafiri, kushughulika na huduma za kila siku za kiofisi.

    10. Kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya kazi kulingana na wakati

    11. Kuandaa na kurekebisha mpango wa huduma wa Chama

    12. Kushughulikia motisha kwa watumishi kwa dhumuni la kuleta ufanisi katika kazi

    13. Kusimamia na kuratibu mikutano ya Chama.


    Kwa ujumla Idara hii inahusika na kazi za kiutawala na mambo mengine binafsi ya Watumishi kwa kushirikiana kwa karibu na ofisi ya Katibu Mkuu.