logo

Tanzania Union of Industrial and Commercial Workers
Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri

logo

SEKTA YA FEDHA

UTANGULIZI

Sekta hii ilianzishwa mwaka 1996 ili kutoa Huduma kwa Wafanyakazi na Wanachama waliopo katika Taasisi za Fedha kama Benki, maduka ya kubadilisha fedha za kigeni, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kampuni za Bima na Taasisi ndogo za Fedha. Huduma hizo ni pamoja na Kuboresha maslahi na mazingira ya Kazi.

MAJUKUMU YA SEKTA

1.Kushiriki Mabaraza ya Wafanyakazi na Mashauriano.

2. Kuhamasisha na kuingiza Wanachama wapya

3. Kushiriki katika mikutano mbalimbali ya wadau

4. Kuzenga na kuzongea katika mapendekezo yanayohusu maboresho ya Sera na Sheria za Kazi

5. Kuwakilisha Wanachama katika Utatuzi wa migogoro ya kikazi.

6. Kujadili na kufunga Mikataba ya Hali Bora (CBA) baina ya Chama na Waajiri.

7. Kuelimisha wafanyakazi kuhusu haki na maslahi yao kazini.

8. Kujenga na kudumisha Uhusiano bora na Wadau wa ndani na nje ya Nchi.